INDHARI: HAYA NI MAONI YA WASOMAJI AMBAYO SI LAZIMA YAAKISI MTAZAMO WA KURUGENZI YA HAKI ZA BINAADAMU NA MAHUSIANO YA UMMA, CUF
atoya
web njema ela jambo moja au mawili; inkosa bendera ya chama ambayo yatakiwa ikae juu kama ilvyokaa picha ya Mh lipumba. pili kama waweza fanya shedow nyuma ya kila page zipattikane rangi za chama. maana kwa sasa ukifugua ata hujui kama ncuf. naminjuavyo kafu yataka ntu akifungua ashtuke kwanza. ila haya yoote nmaoni yangu tu!!
asante
Atoya.
3 09 2008
Ussi Machano (08:56:15)
Sijafahamu kidogo kuhusu tafauti ya itikadi na falsafa. CUF inaposema itikadi yake ni UTAJIRISHO na falsafa yake ni HAKI SAWA KWA WOTE inakusudia kutafautisha dhana hizi mbili. Zinatafautianaje?
4 09 2008
Marry (09:21:55)
Je, haya yote mliyoandika kamadira mmeyafanyia tafiti shirikishi au mnakaa ofisini na kuandika? Nchi hii ni kubwa na ina mambo mengi na watu wengi.
Bila tafiti shirikishi ili utoe sera itakayoweza kutekelezeka ni kama mnacheza na mnawahadaa watanzania. Jaribuni kuwa realistic, especially kwenye kilimo, viwanda na madini.
4 09 2008
Salim Amar Kuku (10:30:49)
Mimi naamini kuwa itikadi ya utajirisho inawezekana sana kwa Tanzania ikiwa rasilimali ziliopo nchini zitasimamiwa ipaswavyo bila kuwaachia MAFISADI akina vijisenti millionea kupora utajiri wa nchi na kuwaacha Wananchi kweupe.
4 09 2008
v99!! (19:52:24)
Tunaupongeza msimamo wenu huu!! Tunakuungeni mkono kwa hali na mali!!
Tunataka kuiona Zanzibar inastawi kimaisha na kuondokana na hali mbaya ya ombaomba iliojitokeza kwa kushirikiana na uchangiaji wa siasa mbovu sisizokuwa na dira, ila kuvimbisha matumbo ya viongozi wake!!
Tunatamani kuiona Zanzibar ilio hai na iliojiweza kujitekemea badala ya kuwa ombaomba!! Mola ibariki CUF iwe ndio dira ya ukumbozi wa ZANZIBAR HURU!!
6 09 2008
Mohammed Abdallah (09:16:12)
Mimi ninamashaka na Sera za C.U.F kwani tangia mwaka 1995 chama hiki kina Wawakilishi na Wabunge waliochaguliwa na Wananchi, lakini ni kwa nini wananchi hawafikiwi na maendeleo hata yale madogo ambaye yanahitaji utendaji mdogo tu wa Mbunge husika.
Kwa mfano hivi sasa njia inayokwenda Mtambile _ Kengeja ina karibu miaka 18 bila ya kufanyiwa ukarabati, wakati Kokoto, mawe na vijana waliotayari kujitolea kuchimba na kufukia pale watakapohitajika na Nyenzo zote muhimu zinapatikana huko huko Kengeja na mara nyingi tumeshuhudia misaada ya Lami ikishushwa, ikiwa ni moja ya nyenzo muhimu za barabara.
Je, maendeleo yatakuja vipi kama Wabunge na Wawakilishi hawana ubunifu wa kupanga hata mipango midogo midogo ya utendaji??
6 09 2008
Asha Mohammed Ali (09:29:12)
Chama cha Wananchi (C.U.F) kina jukumu kubwa sana na wasipoliangalia hili basi chama hiki hakitofikia IKULU mpaka pale jua litakapobadilisha mwelekeo.
Ninakusudia kusema ya kuwa watu wengi hasa Wazanzibar wamepoteza kazi zao, biashara zao, utu wao, mali zao, familia zao kwa matumaini ya kwamba utafika muda wa mavuno kwa chama hiki. Lakini kila siku viongozi walioshikilia nafasi za juu ya chama hiki wanawasaliti wafuasi wao. Utaona badhi yao wanahama C.U.F na kurejea C.C.M au chama chengine. Au kinyume chake chama cha Wananchi (C.U.F) kinawapokea kwa changwe na vigelegele na kuwapa nafasi za juu viongozi waliofilisika kisiasa walioacha vyama vyao, bila ya kujua kuwa hawa ni VIRUS hatari kwa chama. Na hakuna muathirika zaidi wa haya kama si mwananchi.
6 09 2008
Mohammed Abdallah (09:47:05)
Mimi kidogo sijafahamu kwa kina Sera za chama changu cha C.U.F kwa sababu maendeleo si lazima kufika ikulu. Wabunge na Wawakilishi tulionao wanatosha kuwa ni chachu ya kufikia maendeleo. Lakini angalia leo hii ni vitongoji vingapi vya Unguja na Pemba vimeshindwa kuwa na huduma ya Umeme kwa kukosa Transformer, ni vitongoji vingapi havina visima vya maji wa kunywa yaliyo salama. Ni kwanini vishirika vidogo vidogo vya kidini (Waislamu au Wakiristo) wanaweza kutoa misaada ya Transformer na Kuchimba mamia ya Visima vya Kisasa kwa ajili ya wananchi. Je, Sera za C.U.F ndio zinashindwa na mashirika haya kiutendaji?
8 09 2008
Mcha Hassan (20:54:13)
Maalim Seif ametuwakilisha Wazanzibari sote, walio ndani ya nchi na sisi tulio nje huku. Sote tunaamini kwamba Zanzibar yetu kweli ni nchi, ni taifa na ni dola. Hata hivyo, msimamo alioutoa kuwa ni msimamo wa chama chake kuhusiana na kauli ya Mizengo Pinda hautoshi. Lazima sasa CUF iwaongoze Wazanzibari kudai kwa sauti ya juu na kali zaidi haya aliyoyapendekeza Maalim Seif.
Tunafahamu kwamba si Amani Karume wala Shamsi Vuai anayeweza kuitetea Zanzibar kama hivi Maalim Seif anavyowataka waitetee. Kwa hivyo, sasa ni jukumu la CUF kuongoza njia na sio kuionesha tu. Kwa kuanzia, nashauri CUF ikusanye sahihi za Wazanzibari laki moja au zaidi kisha ifunguwe kesi katika Mahakama ya Kimataifa kuhusiana na migogoro ya kikatiba kudai haki ya rais wa Zanzibar kuwa makamo wa rais wa Muungano. Halafu ifunguwe kesi ya kutaka mkataba wa Muungano uwekwe wazi na ujadiliwe kwa mapana na marefu.
CUF isijidogoshe. Ni chama kikubwa, chenye watu na chenye vision na kikiamua kweli, kinaweza kufanya hayo. Na sisi Wazanzibari tutakiunga mkono kwa sababu kinawakilisha matakwa yetu.
Ombi- Nawaomba mututilia “clips” za mihadhara katika internet. Japo kwenye “youtube”. Wenzetu wa Kenya wamefanya hivi na imesaidia sana kuelimisha watu.
Asante
HAKI SAWA KWA WOTE. MAONI YANGU NI NAOMBA HAKIKISHENI RADIO IMEFUNGULIWA KABLA YA UCHAGUZI MDOGO. NA GAAZETI LA FAHAMU LIBORESHWE BADO HALINA MVUTO. AHMADI MACHAKU MOROGORO.
haki sawa kwa wote maoni yangu mimi jee tunasi sikia uchaguzi wa 2010 kupira kwakmputa jamani ninarudiatena hii sikuwibiyana kwasababu ccm wakiyona muwelekeo wa kusnda hawana basi wawo hutafuta kilanjia ya ufisadi kwahiyo hili litizameni kwamakin
Inna lillahi Wainna Illaihi Raajiuun:
Assalaamu Aleikum: Tumezipokea habari za kifo cha Mzee wetu Mzee Shabaani Mloo kwa masikitiko makubwa. Tunamuombea kwake Mwenyezi Mungu amlaze malazi mema. Mwenyezi Mungu ampe kauli thabit, Amghufirie madhambi yake na amueke pamoja na waja wema – Amin. Na wafiwa woote, Mwenyezi Mungu awazidishie subra. Huu ni mtihani wake kwetu sote.
wassalaamu aleiku
Poleni Wazanzibari Kwa kuodokewa na Mzee Mloo
Saturday, 14 March, 2009 1:19 PM
From: “Yussuf Salim”
Asalaama aleykum Wazanzibari
Kwa niaba ya MUWAZA, kwa niaba ya familia yangu na kwa niaba yangu binafsi tunamuombea marehemu Mzee Mloo kauli thabit, aepushwe na adhabu za kaburi, asamehewe makosa yake na alazwe pahala peponi. Amiin !!!
Marehemu Mzee Shaaban Mloo ni katika ya Wazanzibari wa mwanzo walioweza kumkabili Mwalimu Nyerere ana kwa ana na kudai uhuru na mustakbal wa Zanzibar. Bila ya kujali usalama wake, ulwa wake, maslahi yake binafsi hakusita wala kutetereka kwenye msimamo wake wa kutetea haki za Zanzibar ndani na nje ya Muungano.
Marehemu Mzee Mloo leo katutoka lakini katuwachia mifano yake ya ushujaa ya kuikomboa nchi yetu. Katuwachia wajib wa kutekeleza. Katuwachia Wazanzibari wote, bila ya kujali mirengo tofauti, wajib wa kupigania maslahi ya Zanzibar.
Tufuate mifano yake ya kuendelea kupigania Mustakbal wa Zanzibar kwa pamoja.
Inna Lillahi wa Inna Illaihi Rajiuun.
Wasalaalm
Dr. Yussuf S. Salim
A/alaykum,
Itakumbukwa kuwa kuna viongozi wawili hivi sasa ndani ya chama wana conflict wenyewe kwa wenyewe, hayo ni yao lkn kwa upande mwengine wanaharibu taswira ya Chama, nadhani hatua za haraka zinahitajika kudhibiti malumbano haya ili wasikipotezee Chama hadhi na dhamira yake. Hilo lifanyike mapema kama kuna adhabu yoyote inastahili kutolewa kichama basi wawajibishwe haraka. Uamuzi kamili tutauotoa ifikapo uchaguzi unaokuja 2010 tukijaaliwa, maana sisi hatuchagui watu ktk mtazamo wa kimali au madaraka, ikiwa wao hicho ndio chanzo cha ugomvi wao, sisi sera yetu ni ile ile ya Utajirisho lkn si wanamna hii, ni utajirisho katika misingi ya haki na Usawa, ni ajabu kuona watu hawa wanaambiwa wamesoma lkn wanashindwa kutafuta suluhu mpaka wakihusishe chama na masakata yao binafsi. Inakuwaje vikao vyote wanavyofanya wasipate suluhu, mpaka wakimbilie kwenye vyombo vya habari na kuandikiana barua ambazo mimi naziona ni za grade ya kidato cha nne.
Ninakitakia chama mafanikio mema ktk kulishughulikia hili.
a/alaikum
Ninawazo dogo tu, nalo ni kuiomba CUF kufikiria kuanzisha department ya “CUF abroad” nadhani italeta mchango mkubwa kwa kukiendeleza na kukisambaza chama pembe zote za dunia.
(IS SHAME & SAD) TUNAOBA MEDIA ZOTE TANGANYIKA ZIASHANE NA UPOTOFU WA KUIZALILISHA NCHI YETU. ZNZ NI NCHI NA SIO MKOA WALA VISIWA VIDOGO VYA TZ (ISLES)Imetumwa na NGWADU tarehe June 9, 2009 saa 12:16pm katika Siasa
Angalia Mijadala
A/w Takribani wazanzibar wengi tuna sononeka na kuona kishefu x2 tunapo ona wenzetu wa Tanganyika wakitufanyia zarau na kuizalilisha kwa maksudi nchi yetu zanzibar katika media. sisi wazanzibar tunasema upotofu huu wakupotowa watu kwa lengo la makusudi ufe mara moja. katika magazeti mingi ya Tanganyika utaona habari za zanzibar zinawekwa katika mkoa na ukiona nakala nyengine kuhusu zanzibar kama hii hapa shini ya gazeti la mwananchi utaona wanaita ( ISLES) YANI visiwa vidogo. huu wazanzibar tunasema ni upotofu wa maksui na kuizalilisha nchi yetu. iki wa viswa Tanganyika inavyo visiwa vingi lakini sio kama zanzibar zanzbar ni nchi na sio mkoa. na jambo jengine ukiangalia katika utabiri wa hal ya hewa utaskia mkoa wa bwani Tanga,mafya,bwagamoyo na zanzibar kutanyesha mvua za hapa na pale. hii nikuonyesha zahiri kuwa zanzibar sio nchi i mkoa wa bwani wenzetu akili zao zinavyo wapa. kwa hio kama wanashindwa kutamka SEREKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR(SMZ) basi muungano ufe kama walivyo kufa hao mwalounanyisha bila rizadhaa zetu. mana hii ni jeuri na wazanzibar hatuko tayari kuitoa muhanga nshi yetu kua mkoa wa Tanganika. Ikiwa tanganyik kama mujidanganyavyo imekufa basi na muungano ufe kwa vile nyerere na karume waliunanyisha Tanganyika na zanzibar ikawa(Republic of Tanganyika na Zanzibar) sio hishi kilimacho na mazingaombwe ya watanganyika uimeza zanzibar kwa kisingizio cha Muungano fake wa serekali moja yani REPUBLIC OF TANZANIA serekali ya watu wa Tanzania noooooooooo hii ni mfumo wa serekai moja na wazanzibar tusiwe tayari kupigwa shenga na kuisaliti nchi yetu ardhi yetu huu ni ujanja wakitapeli. kwa hio tunaomba baraza la wawakilishi na tasisi zote za zanzibar kuandikia barua vyombo vyote vya media kuwa wasitumie kuondika habari za zanzibar kuweka katika mkoa pamoja na kuishanyanya zanzibar kuwa mkoa wa bwani katika utabiri wa hali ya hewa au kutumia kuwa visiwani (isles) kama watashindwa kuita serekali ya mapinduzi y zanzibar (smz) basi sisi hatuko tayari wazanzibar kutapeliwa nchi yetu.
Don’t be used by politicians, Isles teachers warned
By Mwinyi sadallah
9th June 2009EmailPrintComments
ZanzibarIt has been said that teachers in the Isles lose their jobs after general elections because of their willingness to be used by politicians.
Zanzibar Trade Union Congress (ZATUC) General Secretary Khamis Mwinyi Mohammed gave the remarks at the opening of a one-week course on Labour Laws and Zanzibar Teachers Union Policy.
“The majority of teachers are willing to be used by politicians, ending up being divided due to ideological differences, which often results in their losing their jobs,” he said.
He said the move was against fundamental human rights and good governance, adding that there was no way to deal with the situation.
“If we are to bring this practice to an end, we, as teachers, should refuse to be used by politicians, especially during general elections,” said Mohammed
The SG said many teachers end up in problems due to their involvement in political affairs.
He said this situation faced all teachers who were aligned to political parties.
“We now call on our trade unions to deal with this problem.
We need to have a kind of unity that will work to remove the notion that trade unions are part of the opposition political parties because they differ with the government on many issues,” said Mohammed.
He said ZATUC, in collaboration with ZATU, had already planned to establish an instrument to monitor teachers’ employment.
According to a President’s Committee Report on Workers Claims, a total of 1507 workers were dismissed from government employment including 278 teachers.
The committee was established after the ruling Chama Cha Mapinduzi and the opposition Civic Unitted Front reached a reconciliation pact, during which it was established that many government employees had lost their jobs after the 1995 general election for political reasons.
SOURCE: THE GUARDIAN
Peleka kwa Marafiki
Attachments:
waziri wa nchi ofis ya makamo wa rais mohammed seif hatibu..jpg, 15 KB
mk.bmp, 1008 KB
PALESTINIAN LOSS OF LAND 1946 TO 2005.bmp, 850 KB
ASARI ZA MUUNGANO WAZANZIBAR WANASEMA NIKUBWA KIDINI KULIKO KISIASA.Imetumwa na NGWADU tarehe June 7, 2009 saa 1:53pm katika Siasa
Angalia Mijadala
A/a Wzanzibar katika ufuatiliaji wa faida na hasara za Muungano. wazanzibar walio wengi wamegundua Muungano huu umeasiri sana kizazi cha kizanzibar katika dini na utamaduni wetu asilia wenye ni zamu za kislamu kuliko faida. wengi wanasema sio siasa tu. Zaidi wazanzibar wameasirik katika mfumo mzima wa dini ya kislamu na mila za kislamu katika visiwa vyetu hususani katika kisiwa chetu kikubwa cha unguja. A) zanzibar ninayo ijua mimi ilikuwa ni marufuku kuuza au kununua au kunywa hazarani ulevi waaina yoyote ile. b) zanzibar kulikuwa hakuna nyumba za ukahaba wanawake kuza mili yao C) dini ya kikristian ilikuwa haina nguvu zanzibar na waumini wao zanzibar nzima ilikuwa hawajai hata kanisa moja la kwahani. leo utaona makanisa yamejaa kila kona na hii yote ni mpango malumu na ajenda za siri kuimaliza zanzibar kidini na kiutaa tuni wa mzanzibar. kwa hio mimi nasema wazanzibar tumeasirika sana kidini kuliko kisiasa na kama hatukulivua hili koti la Muungano basi litamaliza kizazi chote cha kizanzibar bila kujua asari zinatokea wapi na zinapenyezwa vipi.
kwa hio tuna aomba nduguzetu wote wa kislamu watusaidie kwa hili ili turudishe zanzibar yetu asilia na hili nijukumu lakila muislamu popte pale alipo.
test access
More watch videos now
You don’t have to sign up, sign in, or sign anything to watch the video. Just click and play! If the link above doesn’t work, copy and paste this url into your browser: http://www.motionbox.com/folders/61390577?affiliate_name=motionbox&;…;...
Motionbox is the easiest way to view, share, and make the most of your personal videos.
Want to use Motionbox to share your own videos securely with friends and family? Learn how it works Peleka kwa Marafiki
Peleka kwa Marafiki
hongereni sana
MAONI YANGU NI KWAMBA IVI RUZUKU ZITOKAZO SERILKALINI ZINAFANYA KAZI GANI KAMA INAFIKIA HATUA MPAKA OFISI YA CHAMA MOROGORO INAFUNGWA KWA KUTOLIPA KODI. KWA CHAMA KAMA CUF NI HAIBNU WAHESHIMIWA.
Nanapenda jambo moja liingizwe katika sera ya Chama kuelekea kipindi cha Uchaguzi mkuu ,jambo lenyewe ni kuzidisha vivutio kwa wananchi katika kuwashawishi kuwepo kwa maendeleo ua kumkomboa mwananchi.
Jambo lenyewe ni kuondosha kodi za viwanja kwa wazalendo ,kuondosha kodi za mashamba kwa wazalendo ,hivi sasa mwananchi mzalendo huwa analipia nyumba yake ya kukaa ,analipia shamba lake analolima ,hizi kodi zipo na kusema kweli inakuwa kama kero,wakati mtu mlo wake wa siku haujui ataupata wapi ,halafu anaongezewa mzigo wa kodi wa pale alipojijengea na pale anapolima,kuna nchi zinawajengea wananchi nyumba na kuwapa bure kuna nchi zinawapa wananchi wake maeneo na kulima bure ,hivyo sioni sababu ya hapa Tanzania kwa mwananchi mzalendo kwa kujenga nyumba na halafu arudi nyumba hiyo akailipie kwa kuwa tu analimiliki nyumba na shamba ,ningewaomba CUF walivalie njuga suala hili liwe moja katika agenda zake za mikutano na wananchi kuwa itawaondolea kodi za viwanja au sijui nyumba ambazo mtu binafsi anamiliki au shamba.Natumai nimeeleweka.Kama mlivyofanikiwa kuipigia makelele kodi ya kichwa basi na sasa muhamishe na kuziandama kodi hizi ambazo ni mzigo mkubwa kwa mwananchi natumai wengi watashawishika na kuikabidhi kura CUF. Mapambano yaendelee kuliko mwanzo CCM hayupo mbali kuanguka.
Assalam alaykum, Mimi kitu cha kwanza naomba haya maoni muyasome na ambayo yana maslahi naomba muyafanyie kazi, nilikuwa nawaulizia wana zanzinei wenzangu jinsi gani tutapata kutoa maoni yetu CUF, ila leo nimepata, zanzinet ni kikundi cha watu wakiwemo watu wanaoishi nje, ambao wanajihusiha na kutaka kuisaidia znz ila tunahitaji serikali imara. Wazanzibari tuko tayari kuwaunga mkono CUF ktk kuleta maslahi ya znz na tanzania kwa ujumla.
Assalam alaykum,
Baada ya utangulizi hapo juu, sasa naomba nichangie, waheshimiwa najua mwajua mengi sisi hatuyajui, na mwajitahid kuona chama kinashika hatamu, lakini mimi napata mashaka na hatua zinazochukuliwa na chama kudhiti njama za ccm, hivi sasa kuna zaid ya watu 3000 hawajaandikishwa ktk majimbo mawili kwa hiyo hadi majimbo yote yaishe takriban watu wapatao 100,000 watakosa haki ya kupiga kura, je sasa waheshimiwa jambo hili munaliachia hivi hivi tu au mushachukua hatua? kumbuka ccm ukiwapa mwanya kidogo tu wanatumianafasi hiyo hiyo, sasa mimi nilikuwa nashauri kila jambo lifanyike kwa wakati, waliokoseshwa haki zao wafuatiliwe hivi sasa tusisubiri hadi wamalize, wakishamaliza kuandikisha watatoa sababu nyengine, na hawa masheha ktk sheria za uchaguzi wametajwa? kama hawajatajwa kwanini munawaachia wanatumika na kuzuia watu haki zao? na pia katika tume ya uchaguzi kuna wajumbe wa cuf mbona sisikii juhudi zao juu ya haya yanayotokea? uchaguzi wa magogoni tunaona jisni ccm ilichukua ushindi? je mikkakati gani tunaichukua?
Mungu ibariki znz, Mungu ibariki tz.
kila la kheri
Mimi nafikiri kabla ya uchaguzi wa 2010 lazima CUF waanzishe kesi za mauaji ya chaguzi zilizopita ili kwafikra zangu, ikiwa akina mkapa na kigengi chake kitaanzwa kuandamwa sasa basi hao akina kikwete wanawezake huenda wa katahadhari kidogo,kwa hivyo nafikiria sana kua CUF wapige moyo konde wasimamie kesi za watu waliodhulumiwa katika chaguzi zilizopita au kama halikufanyika jambo hilo itaonekana kanakwamba munawapuuza wanaopatikana na kadhia hizo.Mimi nafikiri kuupuza mambo kama haya yanaweza kuwavunja moyo wengi wetu katika kusimamia kupigania uhuru wetu na demokrasia ya kweli.
Naungana na wewe bwana hajibwana kwa hili la kuwafungulia kesi hawa madhalim.
hao majambazi kimtindo huo wa vitambulisho naona hatutowaweza maana hiyo ni njama yao ya kijambazi na kudhulumu wazanzibari haki zao hao wenyewe wanalijua kwamba cuf zanzibar ina ushindi mkubwa na hakuna asiyelijua hilo sasa kazi yao nikutumia dola nakutbandikia matatizo lkn yote twamuaachia allah iko siku yao. lkn tujitahidi wazanzibar na wanachama wote tuikomboe zaanzibar maana washaimaliza
KUMTAMBUA KARUME NI KUWASALITI WAANGA WALIOUAWA KWA KUHIAMI CUF:
HAKI SAWA KWA WOTE. KI UKWELI SIWAUNGI MKONO VIONGOZI WOTE WA KITAIFA WALIOSHIRIKI NA KUMTAMBUA KARUME KAMA RAIS WA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR. WAH:LABDA KAMA KUNA UCHAGUZI WA RAIS ULIFANYIKA KARIBUNI NITAUNGANA NANYI LAKINI SIYO ULE WA 2005 AMBAO MATOKEO YAKE YALISABABISHA MAAFA YA WATANZANIA KWA KUIDAI HAKI YAO. WAH: KAMA UONGOZI UMEWASHINDA ACHIENI NGAZI. NI MIMI AHMADI RAMADHANI MACHAKU WA MOROGORO.