“Kamati ya Utendaji ya Taifa imeridhika kwamba kuna hoja za msingi na ushahidi wa kutosha dhidi ya wanachama hao 14 unaoonesha kuhusika kwao na njama hizo.” Read the rest of this entry »
Taarifa ya Kamati ya Utendaji ya Taifa
31 12 2011Comments : Leave a Comment »
Categories : Haki za Binaadamu
SUKZ yaenda mwendo wa mbwa-kachoka?
31 12 2011![smz[1]](http://hakinaumma.files.wordpress.com/2011/12/smz1.jpg?w=300&h=200)
Rais Ali Shein akikutana na serikali watendaji wa serikali yake. Je, watendaji hawa wanaifanya serikali iende mwendo wa mbwa-kachoka: hatua moja mbele, tisa nyuma?
Comments : Leave a Comment »
Categories : Haki za Binaadamu
Muungano sasa uwe wa mkataba, sio wa Katiba
31 12 2011![img_1092[1]](http://hakinaumma.files.wordpress.com/2011/12/img_10921.jpg?w=300&h=224)
Wazanzibari wakiwa katika mjadala wa wazi kuhusu mchakato wa katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA)
Comments : Leave a Comment »
Categories : Haki za Binaadamu
Haki ya misaada ya mafuriko iwe kwa wote
30 12 2011Na Julius Mtatiro
Jana (29 Disemba 2011) tumeimaliza siku nzima kwa kazi ya kuzungukia kambi za wahanga wa mafuriko Dar es Salaam. Nimeongoza ujumbe wa viongozi waandamizi wa chama taifa na wilaya na tumepita katika kambi mbilimbili katika kila wilaya ya Dar es salaam.Zoezi hili limekuja baada ya kupita kwa mara ya kwanza mara baada ya mafuriko. Leo tulikuwa na kazi moja kubwa, KUTOA MISAADA KWA WAHANGA. Katika kila kambi tuliyopita tumewafariji wahanga na kutoa misaada ya UNGA, MCHELE, SUKARI, MAFUTA YA KULA, DAGAA, SABUNI, MAJANI YA CHAI, NGUO, MAHARAGE, n.k. Read the rest of this entry »
Comments : Leave a Comment »
Categories : Haki za Binaadamu
Zanzibar iwe na Benki Kuu yake – Maalim Seif
28 12 2011Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amesema ni muhimu kwa sasa Zanzibar kuwa na benki kuu yake ikiwa inataka kutumia kikamilifu rasilimali zake kujenga uchumi wake. Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, akizungumza katika viwanja vya Kibandamaiti mjini hapa juzi alisema kuendelea kutegemea Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kunainyima Zanzibar kutekeleza mipango yake ya maendeleo kwa ufanisi. Read the rest of this entry »
Comments : Leave a Comment »
Categories : Haki za Binaadamu
Wazanzibari tuungane – Maalim Seif
27 12 2011Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad amesema hana tatizo la wanaotetea serikali mbili lakini kuwepo na mfumo maalumu utakaokubalika na wananchi wote. Alisema wale wanaotetea mfumo wa Serikali mbili, kama ni hivyo yeye hana tatizo. Ila ziwepo Serikali mbili, moja ya Zanzibar na Katiba yake na mambo yake yote, na ya pili ya Tanganyika na Katiba yake na mambo yake yoye. “Halafu tutaamua yepi tunataka tushirikiane na kwa mfumo upi” alisisitiza Maalim Seif. Read the rest of this entry »
Comments : Leave a Comment »
Categories : Haki za Binaadamu

![90247a3d-6a73-4c31-a8e9-de5183d4b3e7[1]](http://hakinaumma.files.wordpress.com/2011/12/90247a3d-6a73-4c31-a8e9-de5183d4b3e711.jpg?w=239&h=300)






Maoni