
Hivi ndivyo Vikosi vya SMZ vinavyowatendea Wazanzibari. Picha hii ilichukuliwa katika harakati za uchaguzi wa 2005
Moja ya maeneo ambayo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imefeli kabisa ni heshima yake kwa haki za binaadamu. Rikodi ya serikali hii katika uwanja huo ni mbaya sana kiasi ya kwamba taasisi nyingi , za ndani na nje, zimewahi kubainisha mara kadhaa kwamba Zanzibar kuna tatizo kubwa la haki za binaadamu. CUF ni chama kilichoundwa katika msingi wa kulinda, kutetea na kudumisha haki za binaadamu na ndio maana katika hotuba yake kwa Baraza la Wawakilishi, Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu Katiba na Utawala Bora, Haji Faki Shaali (MBLW), anaonya juu ya ucheleweshaji wa makusudi wa kesi katika mahakama za Zanzibar kwamba ni dalili kuwa serikali haijali haki za raia na hivyo kuwa miongoni mwa sababu za raia kutokuwa na imani na serikali…
Maoni