
Makamo Mwenyekiti wa CUF, Mhe. Machano Khamis Ali
“Lakini mimi bado naelekea kwa watu wa CCM. Kuna mtego uliowekwa ndani ya viongozi wa CCM. Pinda si mwenda wazimu. Anasema suala hili lizungumzwe na chama cha CCM, maana ndio chama tawala. Waheshimiwa, mimi nataka nikuulizeni nyiye Wazanzibari, hivyo Wazanzibari sasa hatupunguwi milioni moja, CCM wanafika laki nne? Kwa hivyo, ukichanganya wanachama wa CUF na CCM hatuwezi kuwasemea Wazanzibari wote? Bado kuna Wazanzibari hawana uanachama wa CUF wala CCM, lakini bado wana haki na Zanzibar hii. Kama hao wana haki na Zanzibar hii, basi CCM hawana haki ya kuamua hili. Hili haliwezi kuamuliwa na Chama cha Mapinduzi. Hili ni la Wazanzibari wote. Lazima Wazanzibari wote washirikishwe. Matatizo haya haya ya kuyaachia mambo na CCM, ndio CCM wakenda kuamua kwamba Rais wa Zanzibar asiwe Makamo wa Rais.”
Kauli ya CUF kuhusu agizo la Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwamba suala la hadhi ya Zanzibar litamalizwa na CCM… Read the rest of this entry »
Maoni