Tanzania imekosa uongozi ulio makini

23 08 2008

Hamad Rashid Mohammed, Mbunge wa CUF na Kiongozi wa Upinzani Bungeni

Hamad Rashid Mohammed, Mbunge wa CUF na Kiongozi wa Upinzani Bungeni

“….baada ya utafiti huu, sasa tunaweza kusema ni katika mwenendo upi taifa letu linakwenda? Kama tunapoelekea ni pazuri au la? Ikichangiwa na kukosekana kwa Uongozi Ulio Makini, viashiria vya siasa huria ya nchi yetu inajikita katika mambo mengine makubwa, ambayo ni mapungufu ya Katiba, chaguzi mbovu pamoja na ufisadi na umasikini, ambavyo vimewanyima Watanzania ajira na ukuwaji wa uchumi unaofikia angalau asilimia 8%. Mustakabali wa taifa haujengwi kwa maneno mazuri, na tabasamu linalovutia bali ni kwa utendaji ulio makini na unaozingatia matatizo ya Mtanzania.”

Kutoka mada “Changamoto za siasa huria na mustakabali wa taifa-Tanzania: Maoni ya Kambi ya Upinzani Bungeni” iliyotolewa na Mhe. Hamad Rashid Mohammed (Mb), Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, kwa Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia Tanzania (Redet) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, tarehe 20 Agosti, 2008 Read the rest of this entry »





Kukosa nia njema kwa viongozi ndicho kiini cha mgogoro wa Muungano

23 08 2008

Na Juma Duni Haji

Juma Duni Haji, Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Zanzibar

Juma Duni Haji, Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Zanzibar

“Na hata kama hoja yetu (ya kutetea maslahi ya Zanzibar ndani ya Muungano) inaendelea kukataliwa, bado sisi hatuna sababu ya kuiacha eti tu kwa kuhofia kwamba tutatafsiriwa ni vibaraka wa walio nje ya Zanzibar. Watanganyika walikataa kutawaliwa na wakoloni wa Kiingereza wakapigania kujikomboa na mwaka 1961 wakawa huru. Na hata baada ya uhuru huo, wakakataa tena kunyanyaswa na Wakenya ndani ya EAC na mwaka 1967 wakauvunja umoja huo. Wazanzibari nao, kwa upande mwengine, walikataa kutawaliwa na Waingereza na Waarabu na wakadai na kupata uhuru wao takribani katika muda sawa na Watanganyika. Basi ni vyema ikaeleweka kwamba hawatakubali tena kutawaliwa na watu wengine, ukijumuisha hata hao wanaojiita waume zao. Kwamba haki ya kuwa huru ni haki ya kila jamii ya watu!” Read the rest of this entry »