“Kambi ya Upinzani, inalitaka jeshi letu lifikirie kwa kina namna ya kuongeza kasi ya kuleta mapinduzi ya maendeleo katika nchi yetu kama wanavyofanya wenzetu kwa ajili ya kunyanyua uchumi wa nchi zao jambo litakalosaidia kupatikana kwa fedha za kutosha kwa bajeti ya jeshi letu…Kambi ya Upinzani ilikwishashauri jinsi ya kupata vijana wenye vipaji maalum ambao tunaamini kama vipaji hivyo vikitumiwa vizuri jeshi letu litakuwa ndiyo hazina kubwa ya chimbuko la teknolojia mpya na rahisi kwa maendeleo ya watanzania. Jeshi waanze kuwatafuta vijana wenye vipaji tangu wakiwa mashuleni…”
Hotuba ya Mhe. Masoud Abdalla Salim (Mb) Msemaji Mkuu Kambi ya Upinzani Wizara ya Ulinzi wa JKT kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya wizara kwa mwaka wa fedha 2008/2009 Read the rest of this entry »


Maoni