
Timu ya Real Madrid ya Hispania ambayo Rais Kikwete aliahidi kuileta mwaka jana. Iko wapi hadi sasa?
“…miongoni mwa mafanikio ambayo yalisemwa kuwa ni kutokana na ziara za Mheshimiwa Rais nje ya nchi, ni pamoja na ujio wa timu ya mpira wa miguu ya Real Madrid ya Hispania. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitoa tamko la kuthibitisha kuwa timu ya Real Madrid ingelifika Tanzania rasmi kwa michezo ya kirafiki Julai mwaka 2007 ikiwa na msafara wa watu wapatao 80. Hili ni tamko rasmi la Serikali ndani ya Bunge. Kambi ya Upinzani inauliza ujio wa timu hii ni lini? Je, Rais alipotoshwa? Kuna jambo gani hapo? Kama imeshindikana, ni kwanini Serikali inakosa ujasiri wa kulieleza Taifa kilichojiri kama ilivyotamka rasmi na kwa mbwembwe wakati wa kutangaza uwepo wa utaratibu huo?”
Hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani – Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2008/2009 iliyosomwa Bungeni na Mhe. Mwanawetu Said Zarafi (Mb) tarehe 28 Julai, 2008 Read the rest of this entry »

Maoni