Zi wapi zile ajira milioni moja za Kikwete?

11 08 2008

Mhe. Salim Abdallah Khalfan
Salim Abdallah Khalfan, Mbunge wa CUF, Tumbe

”Mheshimiwa Spika, Utafiti wa nguvukazi wa mwaka 2001 ulionyesha kuwa kila mwaka ajira mpya 400,000 zinaanzishwa wakati nguvu kazi laki saba inaingia katika soko la ajira. Serikali ya awamu ya nne iliahidi itaanzisha ajira mpya milioni moja katika kipindi cha miaka mitano wastani wa ajira laki mbili kila mwaka. Waziri ameeleza kwamba katika kipindi cha miezi 18 kuanzia mwezi Julai 2005 hadi Desemba 2007, ajira mpya 412,608 zilikuwa zimepatikana. Ajira 194,325 zimetokana na sekta rasmi na ajira 218,283 zimetokana na sekta isiyo rasmi. Hata hivyo Kitabu cha Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2007 hakina jedwali linaloonyesha ajira hizo na sekta zake. Kitabu hicho kinaonyesha ajira viwandani imeongezeka toka watu 89,316 mwaka 2005 na kufikia watu 91,112, ongezeko la wafanyakazi 1,796 tu. Kwa kadri muundo wa uchumi unavyobadilika ndivyo sekta ya viwanda inavyotegemewa kutoa mchango mkubwa kwa ajira mpya. Aidha, Kambi ya Upinzani inamtaka Mhe. Waziri alieleze Bunge lako tukufu, hizo ajira zaidi ya laki nne ziko sekta gani? Au ajira hizo ni ajira hewa?”

Hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha – 2008/2009 Read the rest of this entry »





Ukuwaji wa uchumi hauonekani kwenye maisha ya watu

11 08 2008
Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mbunge wa Wawi (CUF), Mhe. Hamad Rashid Mohammed

Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mbunge wa Wawi (CUF), Mhe. Hamad Rashid Mohammed

“…..Mtanzania wa kawaida haamini kuwa uchumi unakua kwa sababu haoni matunda ya kukua uchumi. Waheshimiwa Wabunge ambao ndio wawakilishi wa wananchi na wako karibu nao, wanapata shida kupata picha halisi ya ukuaji huu kwa sababu maisha ya Mtanzania wa kawaida yameendelea kuwa duni siku hadi siku…..Ripoti ya Umaskini na Maendeleo ya Watu ya 2007 imebaini kuwa Watanzania wengi wanaona kuwa maisha yao yanazidi kuporomoka siku hadi siku. Wananchi wengi hawaamini kuwa uchumi unakua na maisha ya mwananchi wa kawaida yanaboreka. Wananchi wengi wanaamini kuwa misaada ya nje inawanufaisha wakubwa wa Serikali huku wafanyakazi na wakulima wakiwa wanaambulia  patupu…..”

Hotuba ya Kiongozi na Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, Mhe. Hamad Rashid Mohammed (Mb) kuhusu Bajeti ya Serikali ya Muungano wa Tanzania 2008/2009

Read the rest of this entry »





Tunataka tamko la Serikali kuhusu Ihefu – Mwadini

11 08 2008

“….tatizo la wafugaji waliohamishwa kwenye bonde la Ihefu, Mbarali Mkoani Mbeya ni kubwa. Unyanyasaji

Mhe. Mwadini Abbas Jecha, CUF-Wete

Mhe. Mwadini Abbas Jecha, CUF-Wete

wa wafugaji uliotokea Ihefu mwezi Machi, 2006 kwa kuwaondoa bila utaratibu wala mipango madhubuti na vitendo walivyofanyiwa wafugaji, ambavyo ni kinyume na haki za binadamu bado vimeacha makovu mengi. Wananchi wengi walipoteza mali zao, mifugo, familia na kuumia kisaikolojia. Tume ya Rais, iliyotumia mamilioni ya fedha za Watanzania iliyoongozwa na Mhe. Jaji Chande, hadi leo taarifa yake imewekwa kabatini, na wala Watanzania hawakujulishwa kilichojiri katika ripoti hiyo na wala hatua zilizochukuliwa kwa watendaji waliotekeleza vibaya agizo la Serikali. Kambi ya Upinzani inamtaka Mhe. Waziri atoe Tamko la Serikali kuhusu Taarifa ya Tume/Kamati ya Rais iliyochunguza matukio ya Ihefu ili Watanzania waamini kuwa Serikali yao inawajali.”

Hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2008/2009 Read the rest of this entry »





Fedha za EPA zilipe nauli ya wanafunzi

11 08 2008

Wanafunzi wa Dar es Salaam wakivizia kupanda daladala. Wanafunzi nchini wana tatizo la usafiri na pamoja na hayo nauli za daladala zimepandishwa kutokana na usimamiaji holela wa serikali.

Wanafunzi wa Dar es Salaam wakivizia kupanda daladala. Wanafunzi nchini wana tatizo la usafiri na pamoja na hayo nauli za daladala zimepandishwa kutokana na usimamiaji holela wa serikali.

“Idadi ya wanafunzi wote wa shule za msingi na Sekondari kwa sasa  ni takriban milioni 9 (darasa 1-VII ni 8,31,925 na Sekondari Form I-VI ni 765,672). Hesabu hizi zinajumuisha hata wale walioko katika mashule ya bweni. Tuchukulie kuwa robo tatu yao kuwa wako shule za kutwa ambao ni wanafunzi milioni 6. Waziri wa Fedha alikwishatamka kuwa fedha za EPA hazina mwenyewe na wahusika wamerudisha, basi nusu yake ambao ni shilingi bilioni 66.5 zitumike kama ruzuku ya mafuta, jambo ambalo litasababisha bei ya mafuta kutokupanda na hivyo kisingizio cha bei ya mafuta kupandisha nauli hakitokuwepo tena.”

Taarifa maalum ya Kambi ya Upinzani Bungeni kuhusu maandamano ya wanafunzi wa Dar es Salaam dhidi ya kupandishwa kwa nauli ya daladala Read the rest of this entry »