Tathmini ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete kwa muda wa mwaka mmoja

5 08 2008

Tarehe 21 Desemba 2005, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete aliapishwa kuwa Rais wa nne

Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Haruna Lipuma

Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Haruna Lipuma

wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kushinda uchaguzi mkuu wa 2005. Tarehe 30 Desemba 2005 Rais Kikwete alilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuelezea mambo muhimu ambayo atayasimamia kama Rais wa awamu ya nne. Baada ya kipindi cha mwaka mmoja huu ni wakati muafaka wa kufanya tathmini ya uongozi wa Rais Kikwete kwa kukosoa kwa lengo la kujenga na kutoa ushauri wa kusaidia kuboresha utendaji wa uongozi wake na serikali kuendeleza demokrasia, amani na utulivu wa kweli, na kujenga uchumi utakaokuwa na manufaa kwa wananchi wote na kuwahakikishia wananchi maisha bora kwa kila Mtanzania.

Read the rest of this entry »





Zanzibar ni Nchi na Itabaki kuwa Nchi

5 08 2008
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, akihutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Kibandamaiti Zanzibar 14 Machi, 2008

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, akihutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Kibandamaiti Zanzibar 14 Machi, 2008

“Sasa, mimi hapa natamka kwa mdomo mpana. Natamka asikie Pinda huko aliko, kwamba Zanzibar ilikuwa ni nchi, Zanzibar imekuwa ni nchi, Zanzibar ni nchi mpaka sasa hivi na Zanzibar itaendelea kuwa nchi mpaka yaumul-qiyama (siku ya Kiama). Hapa mimi nimesimama kwenye jukwaa lililo kwenye ardhi ya nchi ya Zanzibar. Sasa kama kuna watu wanaona baya kwa hilo, kama wana uhasidi kwa hilo, watafisidika wao. Zanzibar itakuwepo milele na milele (hata maadui wasipende hilo). Walikuwepo maadui wengi tu wa Zanzibar, lakini leo wako wapi? Wamepita. Na kila mbaya wa Zanzibar atakwenda na maji.”

Hotuba ya Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), MAALIM SEIF SHARIF HAMAD, tarehe 16 Julai, 2008 kujibu kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwamba Zanzibar si Nchi.

Read the rest of this entry »